2.   MAULIDI YA KWANZA

 19

Qaribu Tumwa kuzawa

Babuye alitongowa
Mwanangu mali chukuwa
Shamu nenda kutembeya

20

Ukafanye bia'shara

Na upatapo tijara

Itakuwa ndio bora

Kwa mwana akizaliwa

21

Tutaifanya karamu
Tumshukuru Karimu
Ukimzaa Hashimu
Ni baraka ya
dhuriya

22

Na kumbe hiyo ajali
Na baba yake Rasuli
Wangojana huko mbali
Ajali yamngojeya

23
Alipo kuwa njiani
Anarejea
wat'ani
Aliitwa na
Manani
Na yeye kamwitikiya

24
Alitawafu Madina
Kana kwamba ni kunena:
Namtangulia mwana
Apate pa kufikiya

25
Mwana wangu mtukufu
Yapasa nimsharifu
Atapo kuja tawafu
Nipate kumpokeya

26
Na hivyo yalivyo jiri
Katawafu
Mukhtari
Madina Lianwari
Ndiko aliko jifiya

27
Alipo zawa Hashima
Alikuwa ni yatima
Amina ni wake mama
Ndiye aliye saliya

28
Na babuye ni shaibu
Bwana Abdul Mutt'alibu
Furaha yake a'jabu
Kijana akimjiya  

29
Mzee kajikongoja
Mpaka nyumba ya H'ija
Wah'ijapo wote waja
Na mwana kajibebeya

30
Kangia naye Kaa'ba
Akatoa mat'ilaba
Kaomba Mola kwa h'uba
Kumuombea s'abiya

31
Kaomba kwa mashai'ri
Laini kama h'ariri
Akimwombea
s'aghiri
Mtoto alo mjiya

32
Baa'da kupita juma
Aliandaa walima
Akawaalika umma
Kula na kufurah'iya

33
Hiyo basi ni awali
Maulidi ya Rasuli
Ishike hii qauli
Ishike ishikiliya

34
Maulidi si uzushi
Na tuuwache ubishi
Ni Suna ya Maqureshi
Na Mtume karidhiya

35
Aanzae suna njema
Ujira wake ni mwema
Hadi Siku ya Qiyama
Mtume katuambiya

36
Na ovu mwenye kuzuwa
Ataipata beluwa
Si kwa kuwa hayakuwa
Bali shari katwachiya

37
Hebu soma Qur'ani
Utaona yabaini
Waambiwa Waumini
Mtume kums'aliya

38
Na Mtume kums'ifu
Ni amri takatifu
Kaanza Mola Lat'ifu
Na sisi tunafwatiya

39
Na Mola wetu Muweza
Katuwekea
Ruwaza
Tupate kumuigiza
Mwenye bora ya t'abiya

40
Na pia katuus'iya
Mtume kums'aliya
Na tena kusalimiya
Waumini sote piya

41
Moletu alo tukuka
Amenena bila shaka
Wa Rafaa'na laka dhikraka
Na akumbukwe Nabiya

42
Basi haya Maulidi
Kataka Mola Wadudi
Na sisi hatuna budi
Moletu kumwitikiya

43
Wacha nyoyo zifurah'i
Tusilete ikrahi
Kwa nee'ma ya Ilahi
Aliyo tujaa'liya

44
Na kama wataka sifu
Mpezio mtukufu
Kwa nini sipige dufu
Na rika za kutimiya

45
Na hiyo tena ni Suna
Ya S'ahaba wa Madina
Wakimpokea Bwana
Alipo wafikiliya

46
Lakini nasema basi
Tusikiuke qiyasi
Tukayaleta maa's'i
Katika kufurah'iya

47
Tufurah'i kwa h'ishima
Hili sio lelemama
Wala si kama ni ngoma
Maulidi ya Nabiya

48
Na uwe mnyenyekevu
Tenda mambo kwa wekevu
Usifanye upotovu
Ukaipotea njiya

49
Kwa maneno na vitendo
Na kuufwata mwenendo
Na tuonyeshe mapendo
Kwa Bwana wetu Rasuwa

50
Kama kweli twampenda
Mwenyezi alo tuunda
Yatubidi kuyatenda
Alo tufunza Nabiya

51
Tusiwe tuso a'qili
Tukaifanya
thaqili
Hii Dini ya Rasuli
H'ata ikatuemeya

52
Hii Dini ni nyepesi
Na haina wasiwasi
Mambo yake ni qiasi
Na sote twashuhudiya

53
Tusiitie vikwazo
Kwa kuzua kwa mawazo
Tukaileta mizozo
Isiyo na as'iliya

54
Ni nani mkanya mema
Tulo pewa ni nee'ma
Jamani hivyo si vyema
Vizuri kuvibaniya

55
Maulidi si h'aramu
Kumsifu Mua'dhamu
Wala kufanya karamu
Na watu wakajiliya

56
Wakala walo amini
Pamwe na wao wageni
Fuqara na masikini
Wamshukuru Jaliya   

MAFUNZO

Tunajifunza katika mlango huu kwamba hapana njia ya kusema kuwa kusherehekea kuzaliwa kwa Mtume s.a.w. ni Bida', Uzushi, kwa maana ya kuwa inakwenda kinyume na Dini ya Kiislamu. Bali ikiwa ni jambo lilio anzishwa basi litakuwa katika Sunnatan Hasanah. Wataalamu wa kutegemewa sio wenye kukusanya ilimu tu, bali wale ambao pia wanatumia akili zao na wanatambua lilio bora kulifanya kwa wakati wake na pahala pake. Sherehe za Maulidi ni njia kubwa ya kueneza kwa watu wa kila namna wamjue Mtume s.a.w. na mwendo wake ili wapate kumfuata.