267
Siku moja Mursali
Kaambiwa na Jalali
Upinzani usibali
Watangaziye duniya
268
Tangaza nilo amuru
Alimwambia Ghafuru
Siku hiyo ndiyo Nuru
Izagae kote piya
269
Tumwa naye simuhuli
Hapo hapo kaa'jili
Akalendea jabali
La S'afaa kalikweya
270
Akaweta waungwana
Wakaja wanasongana
Akawambia: Nanena
Na nyinyi mnasikiya
271
Akauliza: Qureshi
Mtaufanya ubishi
Nikinena kuna jeshi
Nyumani linatujiya?
272
Wakanena: Twakubali
Akajibu Mursali:
Vipi hivyo kuwa kweli?
Ni nani ashambuliya?
273
Mnajua tangu kale
Hapana yeyote yule
Awezae kuja mbele
Maka kuja twingiliya
274
Huu mji mtukufu
Hakunaye mpotofu
Akajipaka uchafu
H'arubu kutuleteya
275
Wakajibu: Twaamini
Ukinenawe Amini
Twajua tangu zamani
Urongo hujatwambiya
276
Tena hapo katongowa
Kipenzi chetu Rasuwa:
Niaminini ya kuwa
Ndi Mtume wa Jaliya
277
Nimetumwa kuwajuza
Na Mola wetu Muweza
Mas'anamu kupuuza
Mngu wenu ni Mmoya
278
Haya yangu ms'adiqi
Mfwate Dini ya Haqi
Na kubwa la washiriki
Likazuka lavamiy
279
Ni huyo Abu Lahabu
Ndilo makhuluqu tabu
Liso mjua Wahabu
Kafiri lilo bobeya
280
Hili kubwa la Kufari
Ni a'miye Mukhtari
Ndiye mchimvi wa shari
Kumchimbia Nabiya
281
Likamtusi A'zizi
Likamwita: Mpuuzi
S'ubira yake Mwenyezi
Mbora kuvumiliya
282 Akamtaka S'aburi
Mtumewe as'ubiri
Na
Litakuja angamiya
283
Vituko vyake a'jabu
Huyo Abu Lahabu
Kamkutisha a'dhabu
Sayidi wetu Nabiya
284
Akitesa Isilamu
Akiona ni utamu
Kuwadhili binadamu
Kwa kufwata njema Njiya
285
Na mkubwa wa Juhali
Mwengine Abu Jahali
Huyo khabithi qatili
Ameshinda watu piya
286
Na wako na wengineo
Walio pita upeo
Ole wao Ole wao
Kwa walio tutendeya
287
Hao wakuu wa Nari
Walikaa kudabiri
Wakutishe kila shari
Dini mpya ilo ngiya
288
Wawezao kums'ibu
Wampe nyingi a'dhabu
H'ata mwisho atatubu
Kufuruni tarejeya
289
Mwenye nguvu na u'luwa
Wafanye kumbeuwa
Atakaye kununuwa
Wakatae muuziya
290
Bwana wetu Bubakari
Dini ilipo dhihiri
Alikwenda kukhubiri
Msikitini kangiya
291
Majahili wambaka
Ikawa ni pata shika
Wamkutisha mashaka
Chini wamkanyagiya
292
Kutoka hapo tiati
Akabebwa kitikiti
Si yu hai si maiti
H'ali naye kazimiya
293
Na Bwana wetu Bilali
Muadhini wa Rasuli
Yalo mpata muh'ali
Kuweza yasimuliya
294
Yule mwana wa Khelefu
Kamtesa mtukufu
Akabaki
Mateso kumzidiya
295
Akatatizwa makamba
Wabururwa huo mwamba
Na watoto wamuimba
Na huku wamzomeya
296
Huwekwa kutwa juani
Bila ya nguo mwilini
Na mjiwe kifuani
Wa moto wambabua
297
Aambiwa na Kafiri:
Rejea kwetu ukiri
Jawabu ni kukariri:
Ah'adu ndiye Mmoya
298
Aambiwa: Takuuwa
Ah'adu anatongowa
Mpaka akamwopowa
Abubakari sikiya
299
Katika Waafirika
Bilali ametukuka
H'adhi yake imefika
Kwa walimwengu jamiya
300
Kwani mwenyewe Amini
Kamfanya
S'alati kulinganiya
301
Na wengine Isilamu
A'dhabu
Kuelezea vigumu
Yaliyo kiwafikiya
302
Kwa moto walo uliwa
Na macho kutofolewa
Matumbo kupasuliwa
Na huku wavumiliya
303
Mateso kiwa thaqili
Hwenda hurusha a'qili
Lakini hawakubali
Kufuruni kurejeya
304
Babiye Bwana A'mari
Kababuliwa kwa nari
Na mamiye wakhiari
Kwa madonda kuuliwa
305
A'mari akabaqiya
Mamiye katanguliya
Wa kwanza kushuhudiya
Umati Muh'amadiya
306
Kama qabila wataka
Ni Mama Muafirika
Yamani Mume katoka
Na Mama etwa Sumaya
307
Alo muuwa qatili
Ni huyo Abu Jahali
Akawa ndiye awali
Wa Peponi kuingiya
308
Nimekupeni mithali
Si mingi bali qalili
Mifano ya uqatili
Walio wakitendewa
309
Hao watu Mashahidi
Kwa Dini yao shadidi
Ikawa hapana budi
Kufari kuzingatiya
310
Ikawapasa wawaze
Mbinu gani wageuze
Ili wapate waweze
Hii Dini kuzuwiya
311
Wakaizua shauri
Wamwendee Mukhtari
Wamsemeze vizuri
Aache wake udhiya
312
Na wa kwenda nena naye
Wamchagua mzee
Na jinale niwambie
U'tuba bin Rabia'
313
Akaambiwa Mtume:
Nisikize mwanamume
Haya mambo uyahame
Nimekuja kukwambiya
314
Umekuja tufitini
Kila mtu na mwendani
Twabaki hatujuani
Kwa Dini uliyo zua
315
Watu wetu wagombana
Baba hamjui mwana
H'ishima tena hapana
Sababu wewe wajuwa
316
Sasa wewe ukhiari
Unataka utajiri?
Tutafanya tadibiri
Mali mengi kukweteya
317
Kama wataka tawala
Hilo jambo ni sahala
Ni sasa bila muhula
Sisi ni wako raiya
318
Unataka uraisi
Hilo ni jambo jepesi
Watu wote hata sisi
Tutakuja kwitikiya
319
Kama haja mwanamke
Tafadhali mtamke
Yeyote usishituke
Tutakuja kuleteya
320
Kama unayo maradhi
Mwanangu niwie radhi
Tutafanya la faradhi
Mganga atakujiya
321
Na huyo wako shet'ani
Alo kwingia kichwani
Wachawi wanachuoni
Waweza kumchomoa
322
Myungu yetu ya kijadi
Uiache Muh'amadi
Watuudhi mno h'adi
Unapo ishambuliya
323
Mtume akamjibu:
Nisikize ewe babu
Hayo yote sit'ulubu
Na wala sikuwaziya
324
Mimi langu jambo moja
Na kwa hilo nimekuja
Niwafunze wote waja
La h'aqi kuandamiya
325
Nimekuja kufikiza
Dini ya Mola Muweza
Na sitaraji majaza
Ila kwa Mola Jaliya
326
Mimi kweli nitakalo
Ni jepesi jambo hilo
Mnachie nitendalo
Ujumbe kutimiziya
327
Kushindwa walipo ona
Wakaondoka mabwana
Wakenda kwa muungwana
Mzee wake Nabiya
328
Na huyo Abu T'alibu
Ni a'mi yake H'abibu
Wakenda kumt'ulubu
Amsemeze Rasuwa
329
Na aache wako mwana
Myungu yetu kuikana
Au twache kuyafanya
Tunayo yaqus'udiya
330
Kupita siku i'dadi
Waona mambo kuzidi
Azidisha Muh'amadi
Diniye kutangaziya
331
Kwa Mzee wakarudi
Wakanena: Huna budi
Umzuie waladi
Au vita twanadiya
332
Tutakupiga na wewe
Na alio pamwe nawe
Atanena na mwanawe
Ni hayo alo wambiya
333
Haya mambo ni mazito
Wala qatt'u si matoto
Aliona kama moto
Moyoni unamwingiya
334
Akamwambia Rasuli:
Usinipe uthaqili
Niso weza kuhimili
Mwanangu nikachukua
335
Tena hapo Mukhtari
Machozi yataka jiri
Waweza kutas'awari
Kuh'isi kwake Nabiya
336
Akamwambia: Babangu
Haya mambo siyo yangu
Nda Mwenyewe Bwana Mungu
Mimi ninatumikiya
337
Kama watu wakushinda
Na huwezi kunilinda
Hapana la kulitenda
Ila basi kwendeleya
338
Na Wallahi ninaapa
Lau kama wangenipa
Jua mwezi hapa hapa
Siliachi nilo jiya
339
Siliachi jambo hili
Ila apende Jalali
Akajibu Babe A'li:
Mwanangu nakuachiya
340
Mwanangu nino kupenda
Tenda utalo litenda
Sitoacha kukulinda
Wallahi nakuapiya
MAFUNZO:
Katika sifa kubwa ambayo mwanaadamu yafaa awe nayo ni SUBIRA. Subira huvuta kheri. Kuteswa, kunyanyaswa, kuuliwa, kufungwa, kupokonywa chako - yote hayo ndio mambo ya dharura ya kumpata kila anaye pigania haqi. Yalimpata Mtume Muhammad s.a.w. Na yaliwapata Mitume wote, na yamewapata wote walio tetea haqi. Lakini mwishoe HAQI ndiyo itakayo kuja shinda.