Wanaadamu,
hawajali, ijapo kuwa Hisabu imekurubia, 21:1-3;
taifa moja, 2:213; 10:19;
umbile Mwenyezi Mungu alilo waumbia watu, 30:30;
utukufu unategemea uchamngu, 49:13;
wameumbwa kutokana na jozi moja, 4:1; 39:6; 49:13;
wanaasi kwa ujeuri, 10:23;
Wanaafiqi,
haijuzu kufanya urafiki nao, 58:14-19;
hawamuamini Mungu wala Akhera, 2:8;
hufuata maasi, wakaacha Uwongofu wa Wah'yi, wakipatwa na shida hukujia wapate
ngawira, 4:70-73;
hungojea mambo yawe, wanadhani watamshinda Mwenyezi Mungu, wamezugwa, 4:141-143;
huuza uwongofu kwa upotovu, 2:16;
katika khofu na kiza, 2:19-20;
maradhi ndani ya nyoyo zao, 2:10;
viziwi, mabubu, na vipofu, 2:17-18;
wamelaanika, hawana Imani, wameritadi, wakamatwe na wauwawe, 4:88-89;
wana khofu wasitambulikane, 9:64-65;
wana maneno ya kuvutia, wanaongozwa na ujeuri, 2:204-206;
wanafahamiana wenyewe kwa wenyewe, wapotovu, laana ya Mwenyezi Mungu imewapata, 9:67-69;
wanafanya fisadi, 2:11-12;
wanajidanganya wenyewe, 2:9;
wanakataa kupigania Haqi, 3:167-168;
waongo, na huficha maasi yao kwa viapo, 63:1-4;
waongo na malaghai na woga, 59:11-14;
wapumbavu na hufanya kejeli, 2:13-15;
watakuwa chini kabisa huko Motoni, hawatopata wa kuwanusuru, 4:145;