1. Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.

Rudi kwenye Sura

2. Unajua ya kwamba  hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.

Rudi kwenye Sura

3. Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.

Rudi kwenye Sura

4. Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.

Rudi kwenye Sura

5. Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.

Rudi kwenye Sura