21-
MWISHO
Nalianza
risala hii kwa kunukulu maneno aliyoyasema Father John Mackenzie. Sioni bora
kuliko kumalizia kwa kuyanukulu maneno ya Mkristo mwingine, Geoffrey Parrindar,
aliyeandika katika kitabu chake Jesus in the Quran (Yesu katika
Qur'ani). Amesema:
Inadhaniwa, bila
ya kuzingatia vilivyo, ya kwamba imani zote zinazoaminiwa kwa dasturi, kuwa
msingi wake ni Biblia. Fikra za kumfikiria Mungu zenye asli ya vitabu vya
mbinguni, yafaa zisafishwe na yale mawazo ya Kigiriki yaliyozipamba. Tena
pia ikiwa ilimu ya "Thiolojia" (Ilimu ya Ungu) iambatane na ulimwengu
wa leo, basi ni lazima ielezwe kwa njia yenye maana. Maneno kama Mwana wa
Mungu, Utatu na Uwokofu yapasa yapewe sura nyingine na maana nyingine.
Mawazo ya unabii, na ufunuo, lazima yachunguliwe upya kwa vile ya kuwa hakika
bila ya shaka yo yote Mwenyezi Mungu amemfunulia Muhammad katika Qur'ani.
Tena yapasa tuonyeshe ukarimu zaidi na mafahamiano mema zaidi kwa watu wa dini
nyenginezo. Sisi mara nyingi tunafedheheshwa vile walivyo kuwa Waislamu
wanatuonyesha mfano bora kwa Watu wengine wa Kitabu. Siku zote Wakristo
yahitaji wakumbuke maneno ya Yesu, "Kwa nini kuniita, Bwana, Bwana, na
hamfanyi niyasemayo?"