Kwa
mujibu wa mafunzo ya Mtume Muhammad s.a.w. Imani sio maana yake kuamini
mwengineo atakubebea mzigo wako. Hapana awezae kukuokoa, ila kwa kuwa
anakuongoza njia ya sawa tu. Uokofu uko mikononi mwako mwenyewe.
Qur'ani inasema:
(Qur'ani) Az Zumar 39.7
(Qur'ani) Az Zilzaal 99.7-8
Si
padri, wala kuhani, wala shekhe, wala Yesu, wala Muhammad, atakayetubebea
dhambi zetu au kutufutia dhambi zetu. Imani kama hiyo ni imani ya uvivu
na kujidanganya mwenyewe, kuamini kuwa mateso au kifo cha mtu mwengine kinatosha
kutufutia dhambi zetu sisi. Yesu hakufundisha hayo. Tumekwisha ona
ushahidi wa kutosha katika Biblia kuwa imani hiyo sio aliyofunza Yesu, wala
Manabii wote waliotangulia. Tumenukulu ushahidi kutoka Yeremia
31.29-30, kutoka Ezekieli 18.19-20, kutoka Yohana 9.1-3 na
kutoka Mathayo 18.3. Mafunzo ya imani ya kuwa Yesu kachukua dhambi
za watu kwa kifo chake msalabani kayazua Paulo kwa kuyanukulu kutokana na imani
za kikafiri za kipagani zilizoenea katika Mashariki ya Kati na Ulaya Mashariki
tangu karne za kabla ya kuja Yesu. Attis katika Frigia, Adonis katika
Syria, Dionisa au Bakkus katika Ugiriki, Mithra katika Iran na Osiris na Horus
katika Misri, walikuwa miungu ya uwongo, miungu ya bandia, iliyokuwa na visa
vile vile vya uokozi, na kufutia dhambi kwa kufa kwao na kufufuka kwao kutokana
wafu kama inavyosimuliwa yaliyompitia Yesu. Kwa mfano Attis, mungu wa kipagani
wa Frigia, anaambiwa alizaliwa na bikra Nana, na akiitwa Mwana wa Pekee na
Mwokozi. Aliuliwa chini ya mti wa msonobari kwa kumwagwa damu yake, na
damu yake ikiaminiwa kuwa ilitia rutba katika ardhi na ikaleta maisha
mapya kwa wanaadamu. Kifo chake kilitokea taarikh 24 mwezi wa Machi.
akafufuka kutoka wafu, na kifo chake na kufufuka kwake kulisherehekewa na
wafuasi wake kila mwaka.
Adonis, mungu bandia wa Syria, vile vile alizaliwa na bikra. Yeye pia aliteswa
na akafa kwa kuokoa wanaadamu, na akafufuka kutoka wafu katika nyakati zile
zile za Pasaka.
Dionisa au Bakkus wa Ugiriki akiitwa Mwana wa Pekee wa mungu Jupita.
Alizaliwa na mama bikra 25 Desemba! Kwa wafuasi wake alikuwa ni
Mwokozi. Alijiita mwenyewe Alfa na Omega, yaani wa mwanzo na wa
mwisho. Kisa cha mateso yake kikisherehekewa kila mwaka, na mateso
yenyewe ni kufa, kuteremka jahannam na kufufuka.
Osiris, mungu bandia wa Misri, naye alizaliwa 29 Desemba na mama aliyekuwa
bikra. Alisalitiwa na mtu mmoja aitwae Tifeni na akauliwa. Alizikwa
na akabaki katika jahannam muda wa siku mbili au tatu na masiku yake, na tena
akafufuka kutoka wafu.
Mithra alikuwa mungu-jua wa Waajemi (Wairani). Pia naye kazaliwa na bikra
25 Desemba. Krismasi na Pasaka ndio sikukuu zao muhimu kabisa, kama zilivyokuwa
za dini nyenginezo za kikafiri, kipagani. Hawa Wamithra walikuwa na tambiko
(sakramenti) saba; muhimu kabisa katika hizo ni ubatizo, na Ekaristi (Misa),
ambapo hao washirika hula mkate na hunywa mvinyo, kwa kuwa ndio wanakula nyama
ya Mithra, na kunywa damu yake.
Mwenye kujua ukweli huu lazima ajiulize nafsi yake kuwa Mtakatifu Paulo na
wakuu wa Kanisa wenginewe wamepata tambiko za kufutiwa dhambi kwa damu ya Yesu,
kuzaliwa kwake mwisho wa Desemba, kufa kwake na kufufuka kwake, na Pasaka, na
Misa, na Utatu, kutokana na yeye Bwana Yesu, au kutokana na mila za kikafiri
zilizokuwapo kabla ya Yesu huko Ugiriki, Misri, Syria na Iran?
Leo Tolstoi, Mkristo wa kweli na muaminifu wa Kirusi, ameandika katika risala
yake aliyoita An Appeal to the Clergy (Ombi kwa Mapadri):